Kahama FM

Wanawake, vijana Kahama kupata elimu ya afya ya akili

May 31, 2025, 3:21 pm

Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mboni Mhita akiwa katikati (picha na Sebastian Mnakaya)

Serikali wilayani Kahama imewapongeza na kuwashukuru shirika la suluhisho la wanawake na vijana (Wayds) kwa kuandaa na kuratibu kongamano la afya ya akili.

Na Sebastian Mnakaya

Serikali wilayani Kahama imewapongeza na kuwashukuru shirika la suluhisho la wanawake na vijana (wayds) kwa kuandaa na kuratibu kongamano la afya ya akili lililofanyika wilayani Kahama mkoani Shinyanga.

Pongezi hizo zimetolewa na mkuu wa wilaya ya Kahama Mboni Mhita ambaye alikuwa mgeni rasmi wa kongamano hilo kwa niaba ya Waziri wa afya Jenista Mhagama.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Kahama Mboni Mhita

Sambamba na hayo Mhita amepongeza na kushukuru hatua ya serikali ya awamu ya sita kujenga kituo cha waraibu wa dawa za kulevya Kahama hali itakayowasaidia vijana waliothirika kupata elimu na kutunzwa katika kituo hicho.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Kahama Mboni Mhita

Kwa upande wake mkurugenzi wa shirika la maendeleo kwa wanawake na vijana (WAYDS) Charles Deogratius amesema kuwa kupitia mkutano huo wa afya ya akili wanaanzisha mwamko mpya wa kitaifa ili kutatua tatizo la afya ya akili.

Sauti ya mkurugenzi wa shirika la maendeleo kwa wanawake na vijana (WAYDS) CharleS Deogratius