Kahama FM

Wakulima wa tumbaku, pamba watakiwa kusimamia ubora

March 24, 2025, 3:58 pm

Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mboni Mhita akizungumza katika mkutano mkuu wa 29 wa mwaka wa Chama Cha Ushirika Kahama (KACU) mjini Kahama (Picha Sebastian Mnakaya)

Wakulima wa zao la pamba na tumbaku wametakiwa kusimamia ubora wa mazao hayo kuanzia shambani hadi katika masoko.

Sebastian Mnakaya

Wakulima wa zao la pamba na tumbaku wilayani Kahama mkoani Shinyanga wametakiwa kusimamia vyema ubora wa mazao yao kuanzia katika uzalishaji hadi kuingia sokoni ili kuwa na ubora unaotakiwa.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mboni Mhita wakati wa mkutano mkuu wa 29 wa mwaka wa Chama Cha Ushirika Kahama (KACU) uliofanyika katika manispaa ya Kahama, ambapo amesema kuwa kuzalisha mazao yaliyo bora itawasaidia kuongeza vipato vyao.

Mhita amewataka kuendelea kudumisha umoja na ushirikiano ili kila mkulima kunufaika na ushirika huo, huku wakitakiwa kuzingatia sheria kanuni na taratibu ili kuondoa migogoro isiyokuwa na ulazima.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Kahama Mboni Mhita

Aidha Mhita amesema umefika wakati wa wakulima kulima kilimo cha biashara chenye tija ili kuondokana na hali ya umasikini kwa kuongeza vipato kupitia kilimo hicho, huku serikali ya awmu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassani ikiendelea kuweka mazingira rafiki katika sekta kilimo.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Kahama Mboni Mhita
Mrajisi Msaidizi wa mkoa wa Shinyanga Kakozi Ibrahim

Awali akizungumza katika mkutano huo, Mrajisi Msaidizi wa mkoa wa Shinyanga Kakozi Ibrahim amesema ili kuondokana na migogoro mbalimbali katika ushirika ni kufuata maadili, miongozo, sheria na kanuni zilizowekwa katika uongozi kuanzia kwa wanachama wa kawaida wa vyama mbalimbali vya msingi (AMCOS).

Sauti ya Mrajisi Msaidizi wa mkoa wa Shinyanga Kakozi Ibrahim
Wanachama mbalimbali wa chama kikuu cha Ushirika wilaya ya Kahama wakifatilia mkutano

Ibrahim amewasihi viongozi wa vyama vya ushirika kujiandaa kuendesha shughuli zao kwa njia ya kidikitali na kuzingatia mabadiliko ya tabianchi ili kuepuka hasara na uhakikisha wanachama wanafaidika.