Kahama FM

Wananchi kata ya Nyahanga waomba kujengewa shule ya sekondari

July 15, 2024, 3:40 pm

majengo ya shule ya sekondari ya Nyahanga iliyopo sasa

wameimarisha ulinzi katika maeneo hatarishi kwa kuweka ulinzi wa jeshi la jadi katika nyakati za asubuhi pindi wanafunzi wanapokwenda shuleni.

Na Sebastian Mnakaya

Baadhi ya wananchi wa kata ya Nyahanga Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga wameiomba serikali kujenga shule  nyingine ya sekondari ili kuondokana na vitendo vya uhalifu kwa wanafunzi wanavyofanyiwa wakati wa kwenda shule nyakati za alhifajili kutokana na umbali wa sekondari ya sasa.

Akizungumza na kahama fm  Anjella Mwandu mkazi wa mtaa wa nyahanga wamesema kijana wake amekutana na vikaba wakampora sare zake za shule, viatu na begi huku mwanafunzi Emmanuel Mabula aliyefanyiwa kitendo hicho akielezea tukio hilo.

Sauti ya mzazi na mtoto

Baadhi ya wananchi wa kata hiyo wakizungumza kwa nyakati tofauti wamesema wanashukuru kujengwa kwa shule ya sekondari ya kata ya sasa, huku wakiomba serikali kuongeza shule nyingine kutokana na kata hiyo kuwa na eneo kubwa.

sauti za wananchi

Nae, diwani wa kata ya Nyahanga Pancreas Ikongoli, amesema baada ya tukio hilo wameimarisha ulinzi katika maeneo hatarishi kwa kuweka ulinzi wa jeshi la jadi katika nyakati za asubuhi pindi wanafunzi wanapokwenda shuleni.

sauti ya diwani