Uvinza FM

Tumieni sanduku la maoni kuzisema kero zenu

26 February 2025, 11:48 am

Picha ya sanduku la maoni (picha na Abdunuru Shafii)

Mtendaji wa kata ya uvinza awasihii wananchi kutumia sanduku la maoni kuziwasilisha kero zao pamoja na mapendekezo yao.

Na Linda Dismas

Wananchi wa kata ya Uvinza wameaswa kutumia sanduku la maoni kwa kuwasilisha kero zao.

Mtendaji wa kata ya Uvinza Bw.Edward Amos akiwa ofisini kwakwe wakati akifanya mazungumzo na Uvinza fm(Picha na Linda Dismas)

Hayo yameelezwa na Afisa mtendaji kata ya Uvinza Bw.Edward Amos wakati akifanya mazungumzo na Uvinza fm ofisini kwakwe na kusema kuwa kuna umuhimu mkubwa wa mwananchi kutumia sanduku la maoni kwaajili ya kuwasilisha maoni yake.

Sauti ya mtendaji Bw.Edward Amos

Aidha Bw. Amos amesema kuwa kupitia maoni yanayowekwa kwenye sanduku kunawasaidia wao viongozi kutambua ni changamoto gani wanazokumbana nazo wananchi.

Sauti ya mtendaji Bw.Edward Amos

Pia amewataka wananchi wa kata ya Uvinza kuwa na mazoea ya kutumia sanduku la maoni ili kufikisha mapendekezo na changamoto zao kwa viongozi.

Sauti ya mtendaji Bw.Edward Amos