

March 11, 2025, 3:46 pm
Viongozi wa CCM kata kuacha tabia ya kuwafukuza makatibu wa matawi na mabalozi na badala yake wawafukuze wanaovunja utaratibu wa Chama kwa kuanza kupita kwa wajumbe kwa ajili ya kuwachagua tunapoelekea uchaguzi mkuu
Na Sebastian Mnakaya
Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Shinyanga wametakiwa kuzitatua na kusikiliza kero ndogo ndogo zinazowakabili wananchi katika maeneo yao na wasie chanjo cha migogoro mbalimbali.
Haya yamesemwa leo na mwenyekiti wa Jumuiya wa Wazazi CCM mkoa wa Shinyanga John Siagi ambaye amemwakilisha Katibu mkuu wa Jumuiya hiyo Ally Hapi katika tamasha la kumpongeza Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassani kwa utekelezaji wa ilani ya CCM 2020-2025.
Siagi amesema kuwa kuna badhi ya wanachama kuanza kupita katika kata na majimbo kuomba kura ikiwa bado uchagunzi haujaanza na kuwataka kuacha tabia hiyo ili waliopo madaraki wafanye kazi.
Aidha Siagi amewataka viongozi waliohudhuria katika hafla hiyo waendelea kuwajibika kikamilifu katika majukumu yao ili wawe mfano wa kuigwa katika jamii kwa utekelezaji Ilani ya chama cha Mapinduzi katika miradi mbalimbali ya maendeleo.
Nae, katibu wa CCM wilaya ya Kahama Andrew Chatwanga, amewataka viongozi wa kata kuacha tabia ya kuwafukuza makatibu wa matawi na mabalozi na badala yake wawafukuze wanaovunja utaratibu wa Chama kwa kuanza kupita kwa wajumbe kwa ajili ya kuwachagua tunapoelekea uchaguzi mkuu.
Leo Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Maponduzi (CCM) wilaya ya Kahama imempongeza mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt Rais Samia Suluhu Hassani kwa kuleta fedha nyingi katika mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendelea.