Kahama FM

Wakazi wa Lugela-Mtakuja kuondokana na changamoto ya nishati ya umeme

March 17, 2026, 1:30 pm

Wananchi wakiwa kwenye mkutano na diwani wa kata ya Nyahanga akiambatana maafisa kutoka TANESCO wilaya Kahama

”Huduma ya niashati ya umeme kwa mtaa wa Lugel-Mtakuja unatarajiwa kufika katika eneo hilo hivi karibuni”

Na Sebastian Mnakaya

Wananchi wa mtaa wa Mtakuja kata ya Nyahanga wilayani Kahama mkoani Shinynga, wanatarajia kupatiwa huduma ya nishati ya umeme katika maeneo ambayo bado huduma hiyo haijafika.

Akizungumza katika kikao na wananchi wa Lugela –Mtakuja, wakati wakipatiwa elimu ya namna ya kuunganishiwa umeme katika makazi yao na maafisa kutoka TANESCO, diwani wa kata ya Nyahanga Josephine Kilimba, amesema hatua ya kwanza ni kupatiwa elimu ili umeme unapofika kila mtu awe na sifa za kuunganishwa umeme.

Vifaa vya umeme vya wananchi wa mtaa wa mtakuja wakisubiri kuunganishiwa umeme

Aidha, Kilimba ameliomba shirika hilo kuwasaidia wananchi kupata umeme kwa haraka bila ya kuwa na namba za viwanja ili wakazi hao wafikiwe na huduma hiyo bila ya kuwa na masharti magumu wa upatikanaji wa nishati hiyo.

Sauti ya diwani wa kata ya Nyahanga Josephine Kilimba
Mkuu wa kitengo cha huduma kwa wateja uhusiano na mahusiano kwa umma TANESCO wilaya Kahama Robart Msemo

Mkuu wa kitengo cha huduma kwa wateja uhusiano na mahusiano kwa umma TANESCO wilaya Kahama Robart Msemo, amewataka wananchi hao kujiandaa kupatiwa huduma hiyo ya umeme kwa kufanya maandalizi ya kuweka mifumo ya umeme kwenye nyumba zao.

Sauti ya Mkuu wa kitengo cha huduma kwa wateja uhusiano na mahusiano kwa umma TANESCO wilaya Kahama Robart Msemo
mwenyekiti wa mtaa wa Mtakuja Mohamed Lumala

Nae, mwenyekiti wa mtaa wa Mtakuja Mohamed Lumala ameishukuru serikali kwa jitihada za kuwapatia huduma ya umeme kwa mtaa huo ikiwa ni changamoto ya muda mrefu, huku mkazi wa mtaa huo Dora Marwa akiomba utekelezaji wa mradi huo uwafikie kwa wakati katika maeneo hayo.

Sauti ya mwenyekiti wa mtaa wa Mtakuja Mohamed Lumala na mkazi wa mtaa huo Dora Marwa