Kahama FM

Wafanyakazi wa kampuni ya Costig Holdings ltd wapatiwa mafunzo ya namna ya kujikinga na majanga

February 23, 2026, 12:29 am

Mkurugenzi wa kampuni ya Costig Holdings ltd stewat Bakuju akizungumza katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyakazi

Wafanyakazi wa kampuni ya Costig Holdings ltd iliyopo wilayani Kahama mkoani Shinyanga wametakiwa kujua wajibu wao wawapo kazini pamoja na kuzingatia walichofundishwa na wataalum mbalimbali ili kuongeza uzalishaji zaidi.

Katika mafunzo hayo wataalumu kutoka sekta mbalimabli wakiwemo maafisa kutoka NSSF, Jeshi la zimamoto na uwokaji Kahama, maafisa masoko kutoka Vodacom pamoja na walimu kutoa chuo kikuu Saut wametoa mafunzo mbalimbali kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo.

Agizo hilo limetolewa na Mkurugenzi wa kampuni ya Costig Holdings ltd stewat Bakuju, wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyakazi wa kampuni hiyo, ambapo amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo na kuwa ufanisi wa kazi na wenye tija ili kuongeza masoko na uzalishaji.

Aidha, Bakuju amesema uzalishaji ukiongeza utaweza kusaidia kwa wafanyakazi hao kuongezewa mashahara, huku akiwataka kuwajibika kikamilifu katika utendaji wa kazi pamoja na kujua wanapaswa kufanya nini kazini.

Sauti ya Mkurugenzi wa kampuni ya Costig Holdings ltd stewat Bakuju

Kwa upande wao, baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo, akiwemo Agnes Simon, Boniphace Mass na Gift Peter wameshukuru kupatiwa mafunzo hayo kutoka kwa wataalum mbalimbali ambayo itawasaidia katika utendaji wao wa kazi pamoja na kujikinga na majanga mbalimbali watakayojitokeza.

Sauti za wafanyakazi wa kampuni, akiwemo Agnes Simon, Boniphace Mass na Gift Peter

Naye, mkuu wa kituo cha zimamoto na uwokoaji wilaya ya Kahama Hafidhi Omary, ametoa mafunzo namna bora ya matumizi ya gesi majumbani na viwandani pamoja na namna ya kukabiliana na majango yanapotokea.

Sauti ya mkuu wa kituo cha zimamoto na uwokoaji wilaya ya Kahama Hafidhi Omary

Hata hivyo, kampuni ya Costig Holdings ltd ilianzishwa mwaka 2002, na mapaka sasa inafanyakazi katika mikoa ya Shinyanga, Tabora, Geita, Kagera, Kigoma na singida, huku kwa wilaya ya shinyanga ina wakazi zaidi ya 31.