Kahama FM
Kahama FM
February 14, 2026, 10:57 am

Baraza la madiwa la Halmashauri ya Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga limepitisha rasimu ya makisio ya bajeti shililingi bilioni 70 kwa mwaka wa fedha 2026/2027, fedha zitakazotumika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya Manispaa hiyo.
Bajeti hiyo inatarajiwa kukusanywa kutoka katika vyanzo mbalimbali, ikiwemo mapato ya ndani, ruzuku kutoka serikali kuupamoj na michango ya wananchi.

Akiwasilisha rasimu ya bajetu, mkuu wa idara ya Mipanga wa Manispaa ya Kahama Flora Sangiwa, amesema kuwa rasimu ya bajeti hiyo imepitia hatua zote za kisheria kujadiliwa na kamati mbalimbali za halmashauri, huku ikijikita katika vipaumbe vya elimu, afya na miundombinu ya barabara.
Wakichangia bajeti hiyo, baadhi ya madiwani Manispaa ya hiyo, akiwemo diwani wa kata ya Iyenze Lucas Makulumo na diwani wa kata ya Mhungula Elisha William wamesema kuwa kuna maeneo ambayo ni muhimu, ikiwemo ununuzi wa mitambo ya ujenzi wa barabara yapatiwe kipaumbele katika bajeti hiyo pamoja na kwenye sekta ya afya.
