Kahama FM

Msalala yatoa bilioni moja kwa vikundi vya wajasiriamali

February 8, 2026, 5:23 pm

Mkuu wa wilaya ya Kahama akikabdhi mfano wa Hundi wa shilingi bilioni moja

Mkuu wa wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga Frank Nkinda  amewaasa wanufaika wa mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri kuitumia vizuri kwa kuinua uchumi wao na zisiwe chanzo cha malumbano na ugomvi baina yao.

Nkinda ameyasema hayo wakati akikabidhi hundi ya Shilingi Bilioni moja na milioni kumi na mbili laki mbili na sabini na tatu elfu pamoja na baadhi ya vitendea kazi kwa vikundi vya vijana wanawake na wenye ulemavu katika Halmashauri ya Msalala.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Kahama Frank Nkinda

Afisa Maendeleo ya Jamii Msalala Judica Sumari amesema lengo la mikopo na vifaa hivyo ni kuwezesha makundi hayo kujipatia kipato na kujiendeleza kiuchumi, Huku Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Msalala Six Ibrahim amewataka wanufaika wa mikopo hiyo kurejesha kwa wakati ili kutoa fursa kwa wengine kukopa.

Sauti za Afisa Maendeleo ya Jamii Msalala Judica Sumari na Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Msalala Six Ibrahim

Kwa upande wa wanufaika wa mikopo hiyo Masanyiwa Kazinza pamoja na Lucia Saguda wameishukuru Serikali kwa kuwapatia Mikopo hiyo ambayo inaenda kuinua hali yao ya Uchumi.

Sauti za wanufaika wa mikopo hiyo