Kahama FM

Watakiwa kuwalinda watoto dhidi ya dawa za kulevya, mitandao ya kijamii

July 10, 2025, 4:51 pm

Mwenyekiti wa baraza la wazee manispaa ya Kahama Laurent Nkwabi

Jamii kuchukua jukumu la kuwalinda watoto dhidi ya matumizi ya dawa za kulevya na athari za mitandao ya kijamii kwa kutoa elimu kwa watoto wao’

Na Sebastian Mnakaya

Baraza la wazee manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga limeiasa jamii kuchukua jukumu la kuwalinda watoto dhidi ya matumizi ya dawa za kulevya na athari za mitandao ya kijamii kwa kutoa elimu kwa watoto wao ili kuzuia mmomonyoko wa maadili.

Hayo yamesema na Mwenyekiti wa baraza hilo Laurent Nkwabi wakati akizungumza na Kahama fm katika ofisi za baraza hilo, ambapo amesema kuwa wazazi wanawajibu kuwafatili vijana wao kwa umakini ili wajiingize katika madwa ya kulevya.

Sauti Mwenyekiti wa baraza la wazee manispaa ya Kahama Laurent Nkwabi

Nao Baadhi ya wananchi Katika Halmashauri ya  Manispaa ya Kahama Janeth James na Mussa Raphaeli wamesema kuwa mmomonyoko wa maadili unatokana na kupuuza mila na desturi za kitanzania na kuendekeza mila za kigeni na kwamba kila mtu ana jukumu la kuwalinda watoto hasa watoto wa kike.

Sauti ya wananchi

Kwa upande wao baadhi ya vijana wakizungumza kwa nyakati tofauti akiwemo Aisha Shabani na Clementi Nalindo wamesema kuwa lawama hizo wanawatupia Lawama wazazi la walezi kuwa ndiyo chanzo.

Sauti ya Aisha Shabani na Clementi Nalindo