Kahama FM

Wakulima bora wa tumbaku wapewa zawadi ya pikipiki

June 14, 2025, 10:52 am

Mshindi kutoka chama cha msingi Tulole Heneriko Mhoja baada ya kukabidhiwa pikipiki na kampuni ya Alliance One (Picha na Leocadia Andrew)

Wakulima wa zao la Tumbaku wamekabidhiwa pikipiki baada ya kufanya vizuri katika uzalishaji wa zao la Tumbaku

Na Leocadia Andrew

Kampuni ya ununuzi wa tumbaku Tanzania ya Alliance One imetoa pikipiki kwa wakulima bora wa zao la Tumbaku kwa mkoa wa kitumbaku Kahama, Tabora na Kasulu.

Zoezi la kuwapata washindi hao limefanyika wilayani Kahama kwa kuchezesha droo iliyotoa washindi kumi na tano wa zao la tumbaku.

Akizungumza mara baada ya kuwapata washindi hao afisa mahusiano wa kampuni ya Alliance One Paschal Songalimi amesema kuwa zawadi hizo walizotoa zimezingatia kiwango cha uzailishaji na kwamba lengo la kampuni yao inathamini mchango wa wakulima wa zao la tumbaku.

Sauti ya afisa mahusiano wa kampuni ya Alliance One Paschal Songalimi
Mshindi akikabidhiwa pikipiki baaada ya kuchezeshwa droo kwa wakulima waliofanya vizuri

Akikabidhi zawadi hizo kwa niaba ya Mkurugenzi wa halmashauri ya ushetu Afisa kilimo wa halmashauri hiyo ambaye alikuwa mgeni rasmi katika Bahati nasibu hiyo Vaileth Rutakyamirwa ameipongeza kampuni ya Alliance One kwa kutoa hamasa hiyo kwa wakulima ambayo itawasaidia kuongeza juhudi katika kuendeleza kilimo cha tumbaku.

Sauti ya Afisa kilimo wa halmashauri ya Ushetu Vaileth Rutakyamirwa

Naye mmoja wa washindi kutoka chama cha msingi Tulole Heneriko Mhoja amesema kuwa furaha yake ni kukubidhiwa pikipiki hiyo na ametoa shukrani kwa kampuni ya Alliance One kwa kuendelea kuwajali wakulima wake na kuwataka wakulima wengine kutokata tamaa na wazidi kuzalisha tumbaku kwa ubora.

Sauti ya Mshindi kutoka chama cha msingi Tulole Heneriko Mhoja