Kahama FM

Halmashauri ya Msalala imepokea dozi 82,000 ya chanjo ya Sokota

May 8, 2025, 3:49 pm

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Msalala Rose Manumba akikabidhiwa chanjo ya sokota

watumishi idara ya Mifugo na kilimo katika halmashauri ya Msalala wametakiwa kwenda kutekeleza utoaji wa chanjo hiyo kwa mifugo yote

Na Sebastian Mnakaya

Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama mkoani Shinyanga imepokea zaidi ya dozi 82,000 ya chanjo ya Sokota kwa ajili ya mifugo ya Mbuzi na kondo.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa chanjo hizo mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Msalala Rose Manumba, amewataka watumishi idara ya Mifugo na kilimo tutekeleza utoaji wa chanjo hiyo kwa mifugo, huku mzalishaji wa chanjo hiyo Joseph Mapunda amesema watazambaza chanjo hiyo nchi nzima.

Sauti ya Mkurugeniz wa Halmashauri ya Msalala Rose Manumba na mzalishaji wa chanjo Joseph Mapunda

Mkuu wa idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi halmashauri ya Msalala Mfilinge Abdulikabili amesema kuwa wanachangamoto za ugonjwa Sokota hali inayosabashi kukosa soko ya nje kwa mifugo yao, pamoja na kuishukuru serikali kwa kutoa chanjo hiyo ili kuendana na kuapta soko la uhakika.

Sauti ya Mkuu wa idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi halmashauri ya Msalala Mfilinge Abdulikabili

Kwa upande wake, Daktari wa mifugo kutoka halmashauri ya Msalala Ntano Kilagwile amesema kuwa ugonjwa huo unasababisha vifo vingi kwa mifugo na uzalishaji wake, huku serikali ikiwa na mkatati ya kupambana na magonjwa ya mifugo kwakuwa na kampeni ya mwaka mzima.

Sauti ya Daktari wa mifugo kutoka halmashauri ya Msalala Ntano Kilagwile
Daktari wa mifugo kutoka halmashauri ya Msalala Ntano Kilagwile

Serikali ya awamu ya sita inayoongzwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassani imeendelea kutoa chanjo mbalimbali nchini kwa ajili ya kupambana na magonjwa mbalimbali ya ya mifugo.