Kahama FM

Watendaji katika taasisi za utoaji haki  watakiwa kuzingatia weledi wakati wakitekeleza majukumu yao

February 3, 2025, 6:29 pm

mkuu wa wilaya ya Kahama Mboni Mhita akizungumza katika Kilele cha wiki ya sheria kahama,{picha na Sebastian Mnakaya}

Kilele cha Wiki ya Sheria ni kiashiria cha kuanza rasmi kwa shughuli za Mahakama ambapo kwa mwaka huu maadhimisho hayo yameongozwa na Kauli isemayo “Tanzania ya 2050, nafasi ya Taasisi zinazosimamia haki Madai katika kufikia malengo Makuu ya Dira ya Taifa ya Maendeleo”.

Na Sebastian Mnakaya

Watendaji katika taasisi mbalimbali za kimaamuzi  wametakiwa kuzingatia weledi wakati wakitekeleza majukumu yao kulingana na mipaka na miongozo inavyowaelekeza.

Mkuu wa wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga Mboni Mhita Ametoa rai hiyo leo katika  Kilele cha wiki ya sheria Wilaya ya Kahama ambapo amesema taasisi za kimaamuzi zikifanya kazi kwa kutozingatia mipaka inatengeneza migogoro ambayo haikubaliki.

Sauti ya Mkuu wa wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga Mboni Mhita

Kwa upande wake Hakim Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Kahama Edmund Kente amesema kuwa moja ya Ufanisi katika Taasisi hiyo ni kuendesha Majukumu yake kwa Njia Mtandao ambao umesaidia kupunguza Mrundikano wa Mashauri ambayo hapo awali yalilazimu kutumia muda mrefu.

Sauti ya Hakim Mkazi Mfaidh wa Mahakama ya Wilaya ya Kahama Edmund

Wiki ya Sheria imehitimishwa leo ambapo kwa mwaka huu maadhimisho hayo yameongozwa na Kauli isemayo “Tanzania ya 2050, nafasi ya Taasisi zinazosimamia haki Madai katika kufikia malengo Makuu ya Dira ya Taifa ya Maendeleo”.