Kahama FM

Emanuel Nyambi mwenyekiti mpya chama kikuu Cha ushirika Kahama (KACU)

June 2, 2024, 8:44 pm

Wajumbe wa mkutano Mkuu wa chama kikuu Cha ushirika Kahama KACU picha na Sebastian Mnakaya

wajumbe katika mkutano huo waliopiga kura jumla ni 282 kutoka vyama mbalimbali vya msingi kutoka katika halmashauri tatu za wilaya ya Kahama

Na Leokadia Andrew

Viongozi waliochaguliwa na wajumbe wa chama kikuu cha Ushirika (KACU) wilayani Kahama mkoani Shinyanga wametakiwa kufanya kazi kwa bidii na kuwa waadilifu pamoja na kuzingatia tararibu, kanuni na sheria za ushirika ili wakulima waweze  kunufaika na ushirika huo.

Hayo yamesemwa na Mrajisi msaidizi mkoa wa Shinyanga HILDA BONIFACE, wakati wa uchaguzi wa wajumbe wa bodi na mwenyekiti wa chama hicho, ambapo amesema kuwa wanapaswa kuwatumikia vyema wakulima ikiwa pamoja na kulinda mslahi yao katika kipindi wawapo madarakani

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Kahama MBONI MHITA, amewataka viongozi hao waliochaguliwa kwa kipindi cha miaka mitatu kwa nafasi mbalimbali waende kusimamia kilimo cha pamba pamoja na kwenda na maono ya Rais SAMIA HASSANI katika suala la kilimo.

Sauti ya Mkuu wa wilaya ya Kahama Mboni Mhita

Nae, mwenyekiti mteule EMMANUEL NYAMBI amewashukuru wajumbe wa mkutano mkuu wa KACU kwa kumchagua kwa kura nyingi, nakuwahidi katika kipindi atakachokuwa madarakani atashugulikia changamoto za wakulima pamoja na kusimamia vyema chama hicho kwa manufaa ya wakulima

Sauti ya mwenyekiti Emanuel Nyambi

nafasi ya mwenyekiti ilikuwa na wagombea wawili TANO NSABI aliyepata kura 84 huku EMMANUEL NYAMBI akiwa mshindi kwa kupata kura 198.