Vwawa FM Radio

Serikali yaahidi kuiboresha DIT

January 9, 2026, 10:26 am

Naibu katibu mkuu wizara ya elimu Daniel Mushi wa tatu kutoka kulia. Picha Na Devi Moses

Kwa malengo ya kuongeza ubora wa taaluma

Na Devi Moses

SERIKALI imeahidi kuendelea kuboresha na kuendeleza Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam(DIT) Kampasi ya Songwe ili kuongeza ubora wa mafunzo ya ufundi nchini.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Daniel Mushi,amesema hayo Januari 8, 2026, wakati wa mahafali ya 19 ya duru ya tatu yaliyofanyika katika Kampasi ya Songwe.

Sauti ya Daniel Mushi 1

Mushi ameipongeza DIT kwa juhudi zake za kuwatambua wabunifu na kuwaendeleza ili waweze kuchangia kikamilifu katika maendeleo ya taifa.

Sauti ya Daniel Mushi 2

Awali, Mkurugenzi wa DIT Tanzania, Prof. Preksedisi Ndomba, amewataka wahitimu kwenda kuchapa kazi na kuuza ujuzi walioupata

Preksedisi Ndomba

Akitoa salamu kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mkuu wa Wilaya ya Momba, Mhe. Elias Mwandobo, amewahimiza wahitimu hao kuunda vikundi na kuanzisha kampuni.

Sauti ya Elias Mwandobo