Uyui FM
Uyui FM
9 September 2025, 9:16 pm
Na Zabron G Balimponya
Jamii mkoani Tabora imeshauliwa kutambua na kutumia uwezo uliopo katika kila mtu mmoja mmoja ili uwezo huo usaidie kuleta manufaa kwenye maisha na kujali watu wengine .
Wito huo umetolewa na Felista Michael ambae ni muwezeshaji wa elimu ya stadi za maisha Tabora kutoka shirika la Camfed wakati akizungumza na UFR ambapo amesisitiza kuwa kila mtu ana uwezo ingawa hautumiki kiusahihi

Felista Michael muwezeshaji wa elimu ya stadi za maisha Tabora akiwa studio za Uyui FM Radio
Sauti ya Felista Michaeli
Baadhi ya wakazi wa Manisipaa ya Tabora Elias Habibu na Mariamu Peter wametoa maoni yao juu ya kutambua uwezo hasa kwenye maisha ya kila siku na kutoa ushauli kwa baadhi ya wale ambao hawajatambua uwezo wao
Sauti za Elias Habibu na Mariam Peter
Kwa mjibu wa muwezeshaji wa shirika la Camferd Felista Michael zipo aina 37 za uwezo ambazo binadamu anazo licha ya kuwa ni mara chache mwanadamu kuzitumia kutokana na kutozitambua kwa ufasaha.