Uyui FM

Mradi wa EPPCO kupunguza adha ya maji Ulyankulu Tabora

11 November 2024, 4:38 pm

Baadhi ya watumishi wa Cartas pamoja na mkuu wa makazi ya Ulyankulu.Picha na Ibrahimu

Mradi wa EPPCO utagharimu zaidi ya shilingi milioni 912 hadi kukamilika kwake

Na Zaituni Juma

Serikali ya mkoa wa Tabora imesema kuwa mradi wa EPPCO unaoratibiwa na shirika la Caritas Tabora utakwenda kuwanufaisha wananchi kwa kurahisisha upatikanaji wa huduma ya maji kwa urahisi.

Katibu tawala wa mkoa wa Tabora Daktari John Mboya amesema hayo wakati wa uzinduzi wa awamu nyingine ya mradi huku akimsisitiza mratibu wa mradi huo kukaa kwa pamoja na wakuu wa idara husika ili utekelezaji wake ulete tija kwa jamii.

Daktari Mboya akizungumza na watumishi wa Cartas pamoja na wakuu wa idara.Picha na Zaituni Juma
Sauti ya Daktari John Mboya

Awali mratibu wa mradi wa EPPCO unaoratibiwa na shirika la Caritas Tabora Korduni Titina amesema katika utekelezaji vitachimbwa  visima vitano vipya,ukarabati wa visima 15 na ujenzi wa marambo matano ya kunyweshea mifugo.

Mratibu wa mradi wa EPPCO Korduni Titina.Picha na Rahel Nyabali

Kwa upande wao mganga mkuu wa mkoa wa Tabora Honorata Rutatinisibwa na meneja wa RUWASA mkoa wa Tabora mhandisi Hatari Kapufi wametoa ushauri wao katika utekelezaji wa mradi huo.

Sauti ya mganga mkuu na meneja wa RUWASA Tabora

Nae mkuu wa makazi ya wakimbizi Ulyankulu Jumanne Singani ameeleza umuhimu wa mradi huo ambao umekuwa ukitekelezwa kwa awamu tofauti.

Sauti ya Jumanne Singani

Mradi wa EPPCO umelenga kuimairsha amani na mshikamano kwa jamii zinazoishi  katika eneo la makazi ya Ulyankulu na vijiji jirani ikiwemo vya Mgelela na Songambele mkoani Tabora.

SBOTOP