Uyui FM
Uyui FM
9 September 2025, 8:41 pm
Na Zabron G Balimponya
Imeelezwa kuwa kabla ya kufikia muda wa kustafu kazi ni vizuri kujiwekea mipango ya hakiba ya fedha pamoja na kujiandaa kisaikolojia ikiwa ni pamoja na kujiepusha na ulevi ili kujiweka vyema katika maisha ya uzeeni
Hayo yameelezwa na Afisa kazi mfawidhi mkoa wa Tabora Robert NkungweNkungwe wakati akizungumza na UFR ambapo amebainisha kuwa baadhi ya wastafu husubilia fedha ya mafao ya uzeeni ili kutengeneza maisha jambo ambalo sio sahihi

Afisa kazi mfawidhi mkoa wa Tabora Robert NkungweNkungwe akizungumza na mwandishi wa habari wa Uyui FM Radio
Sauti ya Afisa kazi mfawidhi mkoa wa Tabora Robert Nkungwe
Baadhi ya wazee Tabora wametoa maoni yao wakieleza sababu zinazo fanya wastafu kupitia wakati mgumu katika uzee wao huku wakisisitiza kuwa fedha ya mafao haitakiwi kutumika katika miradi bali ni fedha ya kutumia taratibu.
Sauti za wazee wa Tabora
Kwa mjibu wa Afisa kazi mfawidhi mkoa wa Tabora Robert Nkungweumri wa kustafu kazi huanzia miaka 60 hadi 65.