Kahama FM

TANESCO Kahama yakabidhiwa vitendea kazi

March 29, 2026, 12:23 am

Naibu Waziri wa Nishati, Salome Makamba akikabidhi magari, pikipiki na bajaji kwa TANESCO wilaya ya Kahama (Picha na Sebastian Mnakaya)

Serikali kupitia Wizara ya Nishati imekabidhi vitendea kazi kwa TANESCO Mkoa wa Shinyanga, vikiwemo magari manne, bajaji moja na pikipiki mbili, ili kuboresha utoaji wa huduma za umeme hasa vijijini.

Na Sebastian Mnakaya

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika mjini Kahama, Naibu Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema hatua hiyo inalenga kusogeza huduma za umeme karibu na wananchi na kuchochea maendeleo.

Aidha, Makamba amewahimiza wananchi kuanza kutumia majiko ya umeme, hatua itakayosaidia kuhamasisha matumizi ya nishati safi, salama kwa afya, na rafiki kwa mazingira.

Sauti ya Naibu Waziri wa Nishati Salome Makamba

Salome amesema kuwa wizara ya nishati imesshelea kiasi cha shilingi milioni 85 kwa ajili ya kuimarisha na kuwa na umeme wa uhakika katika wilaya ya kahama pamoja na kuboresha miundombinu mibovu ya umeme.

Sauti ya Naibu Waziri wa Nishati Salome Makamba

 Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa TANESCO Mkoa wa Shinyanga, Mhandisi Benson Mbigili, amesema vitendea kazi hivyo vitasaidia kuongeza ufanisi wa huduma kwa wananchi.