Vwawa FM Radio

Walimu wakuu, tehama Mbozi wapata mafunzo ya SIS

January 5, 2026, 6:39 pm

Baadhi ya wawezeshaji na washiriki wa mafunzo ya mfumo wa SIS. Picha na Devi Moses

Ni mafunzo ya mfumo wa School Information System.

Na Devi Moses

JUMLA  ya walimu 110 kutoka Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe wameshiriki mafunzo ya matumizi ya mfumo wa School Information  System (SIS) yaliyofanyika ukumbi wa Shule ya Sekondari Vwawa Day.

Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo walimu katika ukusanyaji, uhifadhi na usimamizi wa takwimu za shule kwa kutumia mfumo wa kidijitali.

Akizungumza kuhusu faida za mfumo huo, mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Ichenjezya Lukasi Mwambela amesema

Sauti ya mwl, Lukas Mwambela

Kwa upande wake, mtaalamu wa TEHAMA kutoka Shule ya Msingi Ihanda, Joshua Kibona, ameahidi kwenda kuwafundisha walimu wenzake ili kuhakikisha usahihi wa ukusanyaji takwimu.

Sauti ya mwl. Joshua Kibona

Naye Mratibu wa Elimu Kata ya Vwawa, Pelesi Mwakalinga, amefafanua kuwa mfumo wa SIS utakuwa msaada mkubwa katika utekelezaji wa majukumu ya elimu.

Sauti ya Pelesi Mwakalinga

Afisa Elimu  Vifaa na Takwimu wilaya ya Mbozi amesema mafunzo haya ni endelevu kwa walimu wa aina hiyo shule zote

Sauti ya Suma Mwakyusa