Vwawa FM Radio

Machifu Songwe waombea uchaguzi

September 21, 2025, 8:56 pm

Machifu wa Mkoa wa Songwe wakiwa katika dua maalumu ya kuombea uchaguzi. Picha na Devi Mgale

Umoja wa Machifu umefanya dua maalumu kusisitiza amani, utulivu na mshikamano

Na Devi Mgale

UMOJA wa Machifu Mkoa wa Songwe umefanya dua maalumu ya kuombea uchaguzi wa mwaka huu uwe wa amani na utulivu.

Dua hiyo imefanyika Septemba 20, katika Kata ya Mpemba, Wilaya ya Momba, ikiongozwa na Mwenyekiti wa Umoja huo, Chifu Mlotwa Msangawale, pamoja na Katibu wake, Maringa Mkoma. Katika kikao hicho maalumu, wajumbe wameshiriki kwa dua mbalimbali.

Sauti ya chifu Sishe Mgala

Chifu Msangawale ameombea majeshi yawe imara na kuwataka machifu wengine warudi kundini.

Sauti ya chifu Mlotwa Msangawale

Aidha, Katibu wa Umoja huo, Maringa Mkoma, amewakumbusha wajumbe wajibu na majukumu waliyopewa na Chifu Hangaya, ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Sauti ya chifu Maringa Mkoma