Vwawa FM Radio

Watoto wanaookota vyuma chakavu watuhumiwa kwa uhalifu

September 11, 2025, 4:47 pm

Mnunuzi wa vyuma chakavu (mwenye T-shirt ya bluu) akipima vyuma alivyoletewa. Picha Na Devi Mgale

Ni ya utoro, wizi na uharibifu

Na Asteria Kibiki

Watoto wanaojihusisha na vitendo vya kuokota vyuma chakavu katika kata ya Ichenjezya, wilayani Mbozi mkoani Songwe wanatuhumiwa kuongoza kwa utoro shuleni na kujifunza tabia za wizi na uharibifu.

Pamoja na kutoroka shuleni , watoto hao wanadaiwa pia wanajifunza tabia mbaya zikiwamo za wizi wa masufuria na kukata vyuma vya Serikali vikiwamo vibao vinavyoonesha majina ya vitongoji na mitaa.

Ofisa Mtendaji wa Kitongoji cha Ichenjezya, Agness Shitindi, amesema hayo alipozungumza na Vwawa Fm iliyotaka kujua sababu za vibao vingi kuharibiwa katika kitongoji hicho.

Sauti ya Agness Shitindi

Baadhi ya wazazi katika kata ya Ichenjezya  wamekiri kuzumbe katika malezi huku wakitoa wito  kushiriki kikamilifu katika malezi ya watoto wao ili kuzuia vitendo  vya watoto kukatisha masomo na kuzurula mtaani.

Sauti za baadhi ya wazazi