Uyui FM

RC Chacha awasihi wafanyabiashara kujisajili mfumo wa NeST

27 September 2025, 7:14 pm

Na Wilson Makalla

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha amewataka wafanya biashara ndogondogo Mkoani Tabora kujiweka kwenye vikundi na kutumia fursa za kidijitali kwa kuomba tenda kwa wazabuni kwa kutumia mfumo wa manunuzi wa serikali (NeSt) ili kujikwamua kiuchumi kupitia mfumo huo.

Chacha ameyasema hayo Septemba 24, 2025 akiwa mgeni rasmi katika kongamano la wafanyabiashara ndogondogo kutoka wilaya za mkoani humo lililofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Utumishi wa Umma, maarufu Chuo cha Uhazili kilichopo nadani ya Manispaa ya Tabora.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha akizungumza na wafanyabiashara
Sauti ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha.

Kwa upande wao baadhi ya wafanyabiashara na wajasiriamali waliohudhuria kongamano hilo wamesema wamepata ujuzi na maarifa muhimu yatakayowezesha biashara zao kukua huku wakiahidi kujiunga na mfumo wa manunuzi ya serikali na kuomba tenda.

Baadhi ya wajasiriamali na wafanyabiashara wakitoa maoni yao
Baadhi ya wajasiriamali wakifuatilia wasilisho ndani ya ukumbi wa Chuo cha Utumishi wa Umma

Kongamano hilo lililenga hasa kutoa elimu kwa wafanyabiashara hao pamoja na kuwajengea uelewa wa kukua kibiashara kwa kuzikimbilia fursa mbalimbali.