Vwawa FM Radio
Vwawa FM Radio
25/03/2026, 12:11

Lengo la kikao hicho ni kufahamu NGO ipi inafanya nini na wapi.
Na Devi Mgale
MBOZI
Shirika lisilo la kiserikali la DSW limefanya kikao kazi na mashirika mengine kumi yasiyo ya kiserikali (NGO’s) yanayojihusisha na afua za uwezeshaji wa vijana, afya, kupinga ukatili pamoja na uwezeshaji kiuchumi, Machi 24 katika ofisi za Mamlaka ya Mji Mdogo Vwawa, wilayani Mbozi mkoani Songwe.
Akizungumza katika kikao hicho, mwezeshaji kutoka DSW, Peter Owaga, amesema kuwa lengo la kikao hicho ni kufahamu NGO ipi inafanya nini na wapi na kubadilishana uzoefu wa kiutendaji.
Naye Afisa Maendeleo ya Jamii na Mratibu wa NGO’s wilayani Mbozi, Tumpale Mndekesye, ametoa wito kwa mashirika hayo kutoa taarifa za utekelezaji wa miradi kwa mamlaka husika ili kurahisisha ufuatiliaji.
Mkurugenzi wa shirika la EFAD, Elisha Shombe, ameshukuru kwa umuhimu wa mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo ila wafanye kazi kwa weledi.
Aidha, Kaimu Mratibu kutoka shirika la WISCO la usaidizi wa kisheria Christopher Lusoko amesema kubadilishana uzoefu kunawapa urahisi wa kushirikiana.