Vwawa FM Radio
Vwawa FM Radio
February 24, 2026, 8:20 pm

Wanawake Wachoka Kuibiwa Viatu Wakati wa Misiba
Na Mkaisa Mrisho
WANAWAKE wa Vwawa wilaya ya Mbozi mkoa wa Songwe wameibuka na kero ya kuibiwa vitu vyao ikiwemo Viatu au Ndala kwenye Misiba hali inayowalazimu kuviweka Kwapani wakati wa Maombolezo.
Wanawake hao akiwemo Magreth Siwakwi na Prisca Nchinga wameiambia Vwawa Fm Leo kwamba wezi hao ni wanawake wenzao ambao huiba viatu au Ndala Mpya na kuziacha ambazo zimechakaa
Pia wamewataka wanawake ambao wanafanya vitendo hivyo kuwa wastaarabu kwa kufuata kilichowapeleka msibani ili kuepusha kero za aina hiyo
Kwa upande Mwenyekiti wa kitongoji cha Mpakani kilichopo Vwawa Dismas Silayo amesema vitendo hivyo vipo na kwamba baadhi yao huiba mpaka fedha na Simu na kwamba amekuwa akikemea vitendo hivyo ambavyo vimeanza kupungua