Vwawa FM Radio

Wizi Misibani Wawalazimisha Wanawake Kubeba Ndala Kwapani

February 24, 2026, 8:20 pm

Pichani ni Wanawake Wakiwa Kwenye Maombolezo. Picha na AI

Wanawake Wachoka Kuibiwa Viatu Wakati wa Misiba

Na Mkaisa Mrisho

WANAWAKE wa Vwawa wilaya ya Mbozi mkoa wa Songwe wameibuka na kero ya kuibiwa vitu vyao ikiwemo Viatu au Ndala kwenye Misiba hali inayowalazimu kuviweka Kwapani wakati wa Maombolezo.

Wanawake hao akiwemo Magreth Siwakwi na Prisca Nchinga wameiambia Vwawa Fm Leo kwamba wezi hao ni wanawake wenzao ambao huiba viatu au Ndala Mpya na kuziacha ambazo zimechakaa

Sauti za Magreth Siwakwi na Prisca Nchinga 1

Pia wamewataka wanawake ambao wanafanya vitendo hivyo kuwa wastaarabu kwa kufuata kilichowapeleka msibani ili kuepusha kero za aina hiyo

Sauti za Magreth Siwakwi na Prisca Nchinga 2

Kwa upande Mwenyekiti wa kitongoji cha Mpakani kilichopo Vwawa Dismas Silayo amesema vitendo hivyo vipo na kwamba baadhi yao huiba mpaka fedha na Simu na kwamba amekuwa akikemea vitendo hivyo ambavyo vimeanza kupungua

Sauti ya Dismas Silayo