Vwawa FM Radio

TAKUKURU Yagusa Uhai wa Watoto Njiti Songwe

October 16, 2025, 8:02 am

Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Tanzania watatu kutoka (kushoto)Crispin Chalamila akikabidhi mashine kwa Mganga Mkuu wa Mkoa wa kwanza (Kushoto). Picha na Ezekiel Mwinuka

Kwa ajili ya watoto  wachanga wanaozaliwa kabla ya muda (njiti)

Na Ezekiel Mwinuka

Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU nchini Crispin Chalamila amekabidhi vifaa hivyo leo na kwamba vimenunuliwa kwa michango ya watumishi nchini wa Takukuru nchini kwa lengo la kuunga juhudi za Serikali kwenye uboreshaji wa  huduma za afya kwa wananchi.

Sauti ya Crispin Chalamila

Mkurugenzi wa idara ya watoto kutoka hospitali ya Rufaa mkoa wa Songwe Dkt Antia Kakwala amesema hospitali hiyo mpaka sasa imepokea watoto njiti 240 na kwamba mashine hizo zinaenda kuwasaidia kwenye utoaji wa huduma.

Sauti ya Dkt. Antia Kakwala

Mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Dkt.Juma Ramadhani Juma amesema hospitali hiyo kwa sasa inatoa huduma  zote ambazo zinatolewa na hospitali za rufaa hapa nchini.

Pia Mganga mkuu wa Mkoa wa Songwe Dkt.Boniface Kasululu amesema licha ya mkoa wa Songwe kupiga hatua katika kupunguza vifo vya watoto wachanga lakini bado hali hairidhishi.

Sauti ya Dkt. Boniface Kasululu