Vwawa FM Radio

JKT Itaka wafundisha utengenezaji mkaa mbadala

September 21, 2025, 8:40 am

Wahitimu na wakufunzi wa JKT Itaka wakiwa na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Jabiri Makame katika hafla ya kuhitimu mafunzo ya awali ya kijeshi. Picha Na Stephano Simbeye

Ikiwa ni utekelezaji wa agizo la serikali la matumizi ya nishati safi

Na Stephano Simbeye

KIKOSI cha Jeshi la kujenga Taifa (JKT) 845KJ Itaka wilaya ya Mbozi mkoani Songwe kimeanza kufundisha jinsi ya kutengeneza mkaa mbadala kwa kutumia taka za shambani.

Mkuu wa Kikosi hicho, Kanali Gervas Chitola amesema mafunzo hayo yatakuwa yanatolewa kwa askari wapya wanaoingia kwa mujibu wa sheria,

Amesema hayo kwenye hafla  kuhitimu kuwaaga waliomaliza mafunzo ya mujibu wa sharia jana  ambapo mkuu wa Mkoa wa Songwe Mhe Jabiri Makame alikuwa mgeni rasmi.
Aidha kanali Chitola amesema mafunzo hayo yanatolewa kutekeleza agizo la serikali la  kutaka taasisi zinazohudumia watu zaidi ya 100 kutumia Nishati mbadala ili kuhifadhi mazingira.

Sauti ya Gervas Chitola

Aidha Kanali Chitola amebainisha kwamba tayari kikosi hicho kimepata mashine za kisasa zitakazotumika kuandaa mkaa huo unaoweza kutumika pia majumbani.
Naye Mkurugenzi wa mawasiliano wa JKT, Kanali Juma Issa Mlai amesema mafunzo ya awali ya kijeshi kwa mujibu wa sheria yana lengo la kuwandaa vijana, kuwa na moyo wa uzalendo, umuhimu wa kutumia muda vizuri, ukakamavu na ujasiri.

Sauti ya Juma Mlai

Kwa upande wao wahitimu hao wamesema mafunzo waliyoyapata yamewasaidia kufahamu stadi za maisha na yamekuwa chachu na msaada katika maisha Yao, ikiwemo kuwajengea mahusiano na wengine na kuishi kwa upendo.

Sauti ya Mmoja wa wahitimu

Akihutubia kabla ya kufunga mafunzo hayo Mkuu wa Mkoa Songwe Jabiri Omari Makame amewasihi wahitimu hao kuepuka kujiingiza kwenywe makundi mabaya ya matumizi ya mitandao bali waitumie mitandao kama fursa.

Sauti ya Mkuu wa Mkoa Jabiri Makame