Uyui FM

Jamii yaaswa kujifunza lugha ya alama

27 September 2025, 6:46 pm

Na Zabron George

Katika kuadhimisha siku ya Lugha ya Alama Duniani jamii imeshauriwa kuona umuhimu wa kujifunza lugha hiyo ili iweze kusaidia kurahisisha mawasiliano kati ya watu viziwi na wale wasio viziwi.

Wito huo umetolewa na katibu wa chama cha watu wasioona Bahati Sanga wakati akizungumza na UFR ambapo ameongeza kuwa lugha ya alama ni muhimu kwakuwa ndiyo inayotumika kuunganisha jamii hasa kwenye kundi la watu viziwi.

Pichani ni Bahati Sanga wakati akizungumza na UFR
Sauti ya Bahati Sanga

Baadhi ya wakazi wa Tabora wametoa maoni yao juu ya umuhimu wa siku hiyo na kuongeza kuwa luhga hiyo imekuwa msaada katika kukuza mawasiliano hali ambayo inaleta upendo na amani.

Maoni ya wakazi wa Tabora kuhusu kujifunza lugha ya alama

Siku ya lugha ya alama Duniani huadhimishwa kila mwaka ifikapo Septemba 23 ikiwa na lengo la kutambua umuhimu wa lugha hiyo katika kusaidia mawasiliano baina ya mtu asiye kiziwi na mtu ambae ni kiziwi.