Habari za Jumla
29 April 2021, 13:36
Wafanyakazi waeleza matarajio yao kuelekea siku ya wafanyakazi (Mei mosi)
Na; Benard Filbert. Kuelekea maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Mei mosi matarajio ya wafanyakazi wengi nchini ni kuongezewa mishahara na kupandishwa madaraja ili kuboresha utendaji kazi kwa maslahi yao na nchi. Hayo yamesemwa na Bw.Yusuph Mhindi ambaye ni mmoja wa…
29 April 2021, 13:15
Serikali yajipanga kuondoa mgao wa maji Nchini
Na;Yussuph Hans Serikali imesema inaendelea kujipanga kuhakikisha inaondoa adha ya mgao wa Maji kwa Wananchi katika maeneo mbalimbali hapa Nchini. Hayo yamebainishwa leo Bungeni na Naibu Waziri wa Maji Mh MarryPrisca Mahundi wakati akijibu swali la Mbunge wa Ndanda Mh…
29 April 2021, 06:35
Serikali kutunga sheria uvunaji wa viungo
Na;Yussuph Hans. Naibu Waziri wa Afya, Godwin Mollel, amesema kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya upandikizaji wa viungo Nchini, Serikali imeandaa Muswada wa kutunga Sheria itakayoongoza taratibu za uvunaji, utunzaji na upandikizaji wa viungo Ameeleza hayo bungeni jijini Dodoma wakati akimjibu Mbunge…
29 April 2021, 06:17
Zahanati ya Chanhumba yakabiliwa na ukosefu wa dawa
Na; Benard Filbert. Wakazi wa Kijiji Cha Chanhumba Kata ya Handali Wilayani Chamwino wamelalamikia ukosefu wa dawa katika Zahanati ya Kijiji hicho hali inayowalazimu kununua dawa katika maduka ya dawa. Hayo yameelezwa na wakazi wa Kijiji hicho wakati wakizungumza na…
29 April 2021, 06:00
Diwani Nkonko aahidi kuwasaidia vijana kupatiwa mkopo na halmashauri
Na; Seleman Kodima. Diwani wa kata ya Nkonko wilayani Manyoni Ezekiel Samwel amesema ataendelea kupambana na kuhakikisha Vijana katika kata yake wanachangamka na Kupata mkopo unaotolewa Halmashauri kwa kundi la wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ili kujikwamua kiuchumi, kujiongezea…
28 April 2021, 5:33 pm
Wananchi walalamikia miundombinu mibovu ya barabara kwa kukwamisha shughuli zao.
Wananchi wa Mtaa wa Inyanga Kata ya Nyihogo halmashauri ya Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga wameiomba serikali kuwatengenezea barabara ya kutoka Mhungula kwenda mwime ambayo imeharibika kwa kiwango kikubwa na kuwa changamoto kwao. Wakizungumza wananchi hao wamesema suala la miundombinu…
28 April 2021, 5:23 pm
Wafanyabiashara Kazaroho Manispaa ya Kahama wamuomba Mkurugenzi kuvunja masoko.
Wafanyabiashara wa soko la Kazaroho wamuomba mkurugenzi wa Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya soko pamoja na kuyaua masoko yaliyopo pembezoni mwa soko hilo yasiyo rasmi. Wakizungumza baadhi ya wafanyabiashara wa soko hilo wamesema awali walitolewa…
28 April 2021, 2:18 pm
TBS yatoa mafunzo ya vifungashio kwa wajasirimali wa mchele Kahama
Wajasiliamali 100 ambao ni wasindikaji, wauzaji na wasambazaji wa Mchele Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga wamepatiwa mafunzo kuhusu kanuni bora za uzalishaji na taarifa za msingi zinazotakiwa kuwepo kwenye vifungashio na shirika la viwango nchini TBS. Mafunzo hayo yametolewa kwenye…
27 April 2021, 20:47
MARA:UTALII WA NDANI WAONGEZA LICHA YA COVID-19
Idadi ya watalii wa ndani kutembelea na kujionea vivutio mbalimbali imeendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka katiaka hifadhi ya taifa ya Serengeti iliyopo mkoani Mara licha uwepo wa changamoto wa janga la Covid-19 ambapo nchi mbalimbali ulimwengu zinakabiliana na janga hili.…
27 April 2021, 09:21
Wananchi waomba kupatiwa elimu juu ya katiba
NA; Shani Nicoalus Wananchi jijini Dodoma wametoa wito wa kupatiwa elimu juu ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 kutokana na kutoifahamu ipasavyo. Hatua hii imefikiwa baada ya hivi karibuni Halmashauri kuu ya Chama cha…