Habari za Jumla
23 June 2021, 10:58
DC ataka heshima kazini, Narudi kufundisha Madrasa.
Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro Alhaji Majid Hemed Mwanga juni 22 2021 amewataka Viongozi wote Wilayani humo kuwa wabunifu pamoja na kufanya kazi kwa umoja, kushirikiana bila kubaguana wala kudharauliana kwani kwa kufanya hivyo Wilaya itasonga mbele zaidi…
23 June 2021, 10:15
Mradi wa Chujui la Maji Maswa wanufaisha wakazi zaidi ya Laki moja.
Zaidi ya wakazi Laki moja wa Mji wa Maswa na vijiji jirani wamenufaika na Mradi wa Mtambo wa kutibu na Kusafisha Maji. Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Maswa-MAUWASA Mhandisi Nandi Mathias …
23 June 2021, 09:55
Wilaya ya Maswa yaadhimisha siku ya mtoto wa Afrika kipekee.
Jamii Wilayani Maswa Mkoani Simiyu imeaswa kushirikiana na vyombo vya kisheria katika kuhakikisha inatokomeza ukatili kwa watoto. Kauli hiyo imetolewa na Afisa tarafa, tarafa ya Nughu Ndugu Venance Saria kwa niaba ya mkuu wa Wilaya ya Maswa Mh, Aswege Kaminyoge …
22 June 2021, 19:38
Kambi za kujitambua kujithamini na kujiamini ziwe endelevu.
Rai imetolewa kwa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa na shule za sekondari kujenga msingi endelevu wa kuwa na kambi za watoto wa kike kipindi cha likizo lengo ikiwa ni kuwaweka pamoja ili waweze kujifunza masomo mbalimbali ikiwemo lugha…
22 June 2021, 13:27
Wakuu wa wilaya wapya Dodoma wametakiwa kusimamia vema vipaumbele vya Mkoa
Na;Yussuph Hans. Mkuu wa Mkoa Dodoma Mh. Antony Mtaka amewataka wakuu wa wilaya aliowaapisha leo Jijini Dodoma kuhakikisha wanasimamia vyema Vipaumbele vya mkoa na kuleta mabadiliko Chanya. Akizungumza baada ya hafla ya uapisho wa Viongozi hao, Mh Mtaka amesema kuwa…
22 June 2021, 6:39 am
Mh Nassar: Akabidhiwa ofisi na Aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya Bunda Mwl Lydia Bupil…
By Adelinus Banenwa Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mh Joshua Nassar Leo June 21, 2021 amekabidhiwa ofisi na Aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya Bunda Mwl Lydia Bupilipili ambaye amestaafu Akizungumza katika makabidhiano hayo Mh Nassar Amewataka wanabunda wote kuwa wamoja…
21 June 2021, 14:05
Wakuu wa mikoa wapya wametakiwa kusimamia ipasavyo huduma kwa wananchi
Na; Yussuph Hans. Wakuu wa Mikoa walioapishwa hii leo wametakiwa kuhakikisha wanasimamia ipasavyo huduma kwa wananchi katika maeneo wanayoenda kuyatumikia. Wito huo umetolewa na waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Kassim Majaliwa hii leo wakati rais Rais Mh.Samia…
21 June 2021, 10:06
Viongozi wametakiwa kuiga msimamo wa aliyekuwa Rais wakwanza wa Zambia
Na; Benard Filbert. Viongozi katika nchi za Afrika wameaswa kuiga msimamo wa aliyekuwa rais wa kwanza wa Zambia Keneth Kaunda ili waweze kukuza uchumi katika mataifa yao. Hayo yameelezwa na mhadhiri mchambuzi wa masuala ya kisiasa kutoka chuo kikuu cha…
21 June 2021, 9:53 am
TGNP wagawa Radio 100 kwa wananchi wa kata ya Nyambureti Wilayani Serengeti.
By Edward Lucas. Wananchi wa Kata ya Nyambureti, Wilayani serengeti Mkoani Mara, wamelipongeza Shirika la Mtandao wa Jinsia Tanzania TGNP kwa kuwapa msaada wa radio kwa akinamama na wasichana waiishio kwenye mazingira magumu. Wakizungumza baada ya zoezi hilo la ugawaji…
21 June 2021, 9:26 am
Anusurika kifo baada ya kushambuliwa na Nyati
By Edward Lucas Kijana aitwaye Magesa Magori (21) mkazi wa Mtaa wa Tamau, Kata ya Nyatwali Halmashauri ya Mji wa Bunda Mkoani Mara anusurika kifo baada ya kuvamiwa na mnyama nyati wakati akiwa anachunga ng’ombe maeneo ya Tamau. Akisimulia tukio…