Vwawa FM Radio

DC Mbozi atoa onyo kali kwa wavunjifu wa amani kipindi cha uchaguzi

August 9, 2025, 9:12 pm

Baadhi ya viongozi wa dini na vyama vya Siasa walioshiriki kikao cha mapitio ya ratiba ya uchaguzi katika wilaya ya Mbozi. Picha na Stephano Simbeye

viongozi wa vyama vya siasa, viongozi wa dini na wadau wengine wa uchaguzi wamekutana Mbozi kuweka mikakati ya kuhakikisha uchaguzi mkuu unafanyika kwa amani na haki, huku DC Hamad Mbega akitoa onyo kali kwa wavunjifu wa amani

Na Stephano Simbeye

Serikali wilayani Mbozi, mkoa wa Songwe, imesema haitamvumilia mtu yeyote atakayejaribu kuvuruga amani katika kipindi hiki cha uchaguzi.

Kauli hiyo imetolewa Agosti 8 mwaka huu na Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. Hamad Mbega, wakati akitoa salamu za serikali katika kikao cha kupitia ratiba ya Uchaguzi Mkuu iliyotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi. Kikao hicho kimehusisha viongozi wa vyama vya siasa, viongozi wa dini na wadau wengine wa uchaguzi.

Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Karl uliopo mjini Vwawa. Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mbega amesema:

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. Hamad Mbega akitoa onyo kali kwa wavunjifu wa amani kipindi cha uchaguzi

Aidha, Mbega amesema uchaguzi ni takwa la kikatiba na ni lazima ufanyike ili kupata viongozi watakaoongoza kwa kipindi cha miaka mitano ijayo baada ya muda wa uongozi kumalizika. Alisisitiza hakuna mtu yeyote mwenye uwezo wa kuzuia mchakato huo.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. Hamad Mbega

Kwa upande wake, Kiongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) wilaya ya Mbozi, Enock Mwalukasa, amesema matatizo mengi ya uchaguzi huanzia kwa mawakala hivyo alipendekeza mawakala waapishwe katika maeneo yao ya kata.

Kiongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) Wilaya ya Mbozi, Enock Mwalukasa akizungumzia changamoto za uchaguzi
Baadhi ya viongozi wa dini na vyama vya Siasa walioshiriki kikao cha mapitio ya ratiba ya uchaguzi katika wilaya ya Mbozi. Picha na Stephano Simbeye

Akizungumzia suala la uchukuaji na urejeshaji wa fomu, Mwalukasa ameonya dhidi ya mchezo wa kufunga ofisi za watendaji uliowahi kutokea katika chaguzi zilizopita, akisisitiza kwamba jambo hilo lisijirudie mwaka huu.

Kiongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) Wilaya ya Mbozi, Enock Mwalukasa akizungumzia zoezi la uchukuaji wa fomu

Baadhi ya viongozi wa vyama vya Siasa walioshiriki kikao cha mapitio ya ratiba ya uchaguzi katika wilaya ya Mbozi. Picha na Stephano Simbeye

Viongozi wa madhehebu ya dini wamesema wanatarajia uchaguzi wa mwaka huu utakuwa wa haki, amani na utulivu, huku wakiongeza kuwa wamekuwa wakiombea hali hiyo idumu.

Msimamizi wa Uchaguzi wa Majimbo ya Vwawa na Mbozi, Danny Tweve, amesema tume imejipanga kuhakikisha uchaguzi unakuwa huru na wa haki akiongeza kuwa hakutakuwa na visa vya kufunga ofisi za umma kwa visingizio vyovyote, na kuwataka wadau kutoa taarifa mapema iwapo wataona viashiria vya hali hiyo.