Vwawa FM Radio

Abiria wajadili uchafu wa madereva wa bodaboda Mbozi

June 5, 2025, 1:57 pm

Baadhi ya bodaboda zikiwa kwenye kituo cha Ichenjezya Mbozi. Picha na Anyisile Fredy

Wadai kukerwa na harufu mbaya, mwenyekiti wa madereva atoa ya moyoni

Na Anyisile Fredy

Baadhi ya abiria  wa bodaboda na bajaji mjini Vwawa Mbozi mkoani Songwe wameendelea kuzungumzia kero wanazopata kwa madereva wachafu wa vyombo hivyo.

Akizungumzia suala hilo, abiria Daniel Ngajilo kutoka Ichenjezya amesema baadhi ya madereva wanavaa makoti machafu yanayonuka kwa siku nyingi bila kufuliwa.

Sauti ya Daniel Ngajilo abiria wa bodaboda

Naye dereva mstaafu wa bodaboda wilayani Mbozi, Jack Mponda amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na ameshauri kutolewa kwa elimu ya usafi mara kwa mara wanapokutana vijiweni.

Amesema abiria wengine wanatamani washuke kwenye pikipiki ama bajaji kutokana na harufu mbaya ya dereva jambo ambalo halipendezi kwa madereva wa bodaboda ama bajaji.

Sauti ya Jack Mponda dereva mstaafu

Akizungumzia changamoto hiyo, Mwenyekiti wa madereva wa bodaboda wa kijiwe namba 10 Vwawa, Saidi Lwenje amekiri kuwapo kwa baadhi ya madereva wasiozingatia usafi.

Aidha amewataka madereva kuzingatia usafi wa mwili na mavazi kila siku ikiwa ni pamoja na kuoga asubuhi na kuvaa nguo safi.

Sauti ya mwenyekiti wa madereva wa bodaboda wa kijiwe namba 10 Vwawa, Saidi Lwenje