Waamini wa kanisa la Last Church of Tanzania Wakigawa bidhaa kwa wahitaji.
Vwawa FM Radio

Last Church of Tanzania lagusa wengi kwa msaada wa kipekee Mbozi

June 1, 2025, 11:20 am

Waamini wa Kanisa la Last Church of Tanzania wakiwa tayari kukabidhi baadhi ya mahitaji kwa watu wasiojiweza mjini Vwawa. Picha na Anyisile Fredy

Kanisa la Last Church of Tanzania limeendesha zoezi la kugawa misaada ya bidhaa muhimu kwa wahitaji wilayani Mbozi, likisisitiza kuwa huduma hiyo itaendelea kila mwezi.

Na Anyisile Fredy

Askofu wa Kanisa la Last Church of Tanzania, David Sichone, amesema utoaji wa msaada kwa wahitaji ni sehemu ya utume wa kiroho wa kanisa hilo, akisisitiza kuwa huduma hiyo itaendelea kila mwezi na wanafanya hivyo kama maandiko yasemavyo

Sauti ya Askofu David Sichone

Mmoja wa walionufaika, Bi. Sifa Munjwanga, amesema msaada huo umekuja kwa wakati sahihi na kuleta faraja kwao. Ameongeza kuwa matukio kama haya yanawapa matumaini mapya.

Sauti ya Sifa Mujwanga

Msaada huo ni ishara ya upendo na mshikamano wa kidini, ukiibua hamasa ya kuwasaidia wenye uhitaji bila kujali tofauti za kiimani.