Vwawa FM Radio

Wanandoa watakiwa kuvumiliana

May 7, 2025, 12:46 pm

Moja ya ishara ya Ndoa ni pete. Picha na Pili Mwang’osi

Malengo ni kupunguza ndoa kuvunjika

Na Pili Mwang’osi

TAASISI zinazofungisha ndoa Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe, zimewataka wanandoa hususan vijana kuwa wavumilivu ili kupunguza wimbi la ndoa kuvunjika.

Ofisa Tarafa ya Vwawa, Wilaya ya Mbozi, Edward Lugongo , ametoa wito huo alipozungumza na Vwawa FM Mei 6, 2025. Lugongo amesema wanandoa wanapaswa kuvumiliana kutokana  na ukweli kwamba kila mmoja ana madhaifu.

Sauti Edward Lugongo

Naye Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Usharika wa Vwawa,  Iku Mwakisimba amezungumzia moja ya chanzo cha ndoa nyingi kuvunjika.

Sauti Iku Mwakisimba 1

Mchungaji Iku ametoa wito kwa wanandoa kupenda mafundisho pamoja na kufuata kanuni za Mungu kuhusu ndoa huku akisisitiza  vijana kuacha tamaa

Sauti Iku Mwakisimba 2

Aidha naye Mwinjilisti wa kanisa hilo  Ambwene Mwanyerere  na katibu wa wanawake kanisa la  EAGT Sayuni wametoa maoni yao.

Sauti Mwanyerere na mrs Siwiti