Uyui FM

Utelekezaji wa familia unavyoathiri malezi ya watoto

31 March 2026, 12:09 pm

Mtangazaji wa UFR Mwanne Jumaa akifanya mahojiano na Bi. Tausi.Picha na Mohamed Habibu

Makala hii inaelezea mwanamke ambae aliyetelekezwa na mumewake baada ya kupata ulemavu na kusababisha mzigo wa malezi kwa mzazi mmoja.

Na Zaituni Juma akishirikiana na Nicholaus Mwaibale

Bi Tausi ni mama wa watoto watatu mkazi wa Manispaa ya Tabora, ambaye mwaka 2018 alipata ajali ya kuanguka na kumsababishia kuwa na ulemavu wa kudumu, na sasa anasaidiwa kufanya kila kitu na binti yake, lakini kwa muda wote huo amekuwa akilea familia peke yake kutokana na mwenza wake kumtelekeza.