Uyui FM
Uyui FM
27 September 2025, 5:50 pm
Na Kimwaga Shaban
Mashindano ya ligi kuu Daraja la kwanza Taifa ya mchezo wa Pete ambayo yanafanyika katika Mkoa wa Tabora kuanzia Jumamosi Septemba 26, 2025 katika viwanja vya shule ya Tabora wasichana (Tabora Girls).
Akizungumza na UFR Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Pete Mkoa wa Tabora Bi. Maimuna Abbas amesema mashindano hayo ni makubwa kufanyika katika mkoa wa Tabora pia ameahidi kuukuza mchezo huo katika Mkoa huu.

Kwa upande wa katibu wa wa chama hicho Mwalimu Mwajuma Yusuph amesema hadi sasa maandalizi kwa upande wa Mkoa yamefikia hatua za mwisho lakini amewatoa shaka washiriki wote kuwa hadi ifikapo jioni ya leo kila kitu kitakuwa kimekamilika kwa asilimia mia.

Mashindano hayo yanazikutanisha timu 15 kutoka katika mikoa mbalinbali huku mkoa wa Tabora ukiwa na timu mbili kutoka katika wilaya ya kaliua na Nzega.