Uyui FM

Jeshi la polisi Tabora lahimiza kampeni za kistaarabu

27 August 2025, 7:50 pm

Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora, kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi Richard Abwao akizungumza na Uyui FM Radio akiwa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Tabora.

Jeshi limejipanga kuwadhibiti watakao kiuka sheria na taratibu katika kipindi cha kampeni

Zaituni Juma

Jeshi la polisi mkoa wa Tabora limejipanga kikamilifu kuhakikisha zoezi la kampeni kuelekea uchaguzi mkuu linafanyika kwa amani na utulivu.

Akizungumza na UFR Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora, kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi Richard Abwao amesema, jeshi hilo limejipanga kuwadhibiti watakao kiuka sheria na taratibu katika kipindi cha kampeni.

Sauti ya Kamanda Richard Abwao

Kamanda Abwao amewataka wananchi kushirikiana na Jeshi la polisi kwa kutoa taarifa za wahalifu.

Sauti ya Kamanda Abwao akihimiza wananchi kutoa ushirikiano

Badhi ya wananchi wametoa rai kwa  jamii kushiriki kampeni kwa amani na kusikiliza Sera za wagombea ili kupata kiongozi bora.

Sauti za wakazi wa Tabora wakitoa maoni yao

Kwa mujibu wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), kampeni zinatarajia kuanza mnamo Agosti 28 hadi Oktoba 28 mwaka huu.