Uyui FM

RC Chacha akabidhi trekta mbili chuo cha AMUCTA

14 June 2025, 10:19 am

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha (wa pili kutoka kushoto) akikata utepe wakati wa kukabidhi trekta mbili kwa uongozi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Askofu Mkuu Mihayo Tabora. Picha na Mohammed Habibu

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha amekabidhi trekta hizo kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe ikiwa ni katika kutimiza ahadi aliyoitoa chuoni hapo.

Na Zaituni Juma

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Matiko Chacha amekabidhi trekta mbili (2) kwa Chuo Kikuu Kishiriki cha Askofu Mkuu Mihayo Tabora (AMUCTA) wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika tarehe 10 Juni, 2025 chuoni hapo.

‎Makabidhiano hayo ni utekelezaji wa ahadi ya Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe aliyoahidi tarehe 23 Novemba, 2024 alipohudhuria mahafali ya kumi (10) ya chuo hicho ili kuchangia mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wa elimu ya juu.

Sauti ya Mkuu wa mkoa wa Tabora, Paul Chacha.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha akitoa salamu za Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe. Picha na Mohammed Habibu.

Mkuu wa Chuo cha AMUCTA, Profesa Juvenalis Asantemungu amesema trekta hizo zitatumika katika kuandaa mashamba darasa kwa ajili ya wanafunzi wa chuo hicho.

Sauti ya Mkuu wa chuo cha AMUCTA Profesa Juvenalis Asantemungu.
Mkuu wa chuo cha AMUCTA Profesa Juvenalis Asantemungu akishukuru baada ya kupokea trekta. Picha na Mohammed Habibu.

Lengo la Wizara ya Kilimo na serikali ni kuchangia uendelezaji wa mafunzo kwa vitendo katika sekta ya kilimo na kuongeza soko la ajira kwa wahitimu wa elimu ya juu nchini.

Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha AMUCTA wakifuatilia kwa makini hafla ya makabidhiano ya trekta. Picha na Mohammed Habibu.