Savvy FM
Savvy FM
January 14, 2026, 5:08 pm

Zaidi ya vijana 200 jijini Arusha wameanza kunufaika na mradi wa kuwawezesha kiuchumi kupitia mpango wa kukopeshana pikipiki kwa gharama nafuu, uliozinduliwa na Umoja wa Maafisa Usafirishaji jijini Arusha kwa kushirikiana na kampuni ya TVS (Trust Value Service), lengo likiwa ni kuongeza ajira, kipato na ustawi wa vijana wanaojishughulisha na usafirishaji wa pikipiki.
Na Mariam Malya
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo, Katibu wa Boda Boda Mkoa wa Arusha, Bw. Richard Magembe, kwa niaba ya maafisa usafirishaji amesema mradi huo umeanza kuwanufaisha wanachama 200, ambapo pikipiki hizo zimetolewa kwa mfumo wa kukopeshana kwa masharti nafuu. Amesema pikipiki hizo ni za majaribio zilizoanza kutumika mapema mwezi Desemba mwaka jana, hatua inayolenga kupima ufanisi wa mradi kabla ya kuupanua zaidi.
Akikabidhi rasmi pikipiki hizo, Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Mhe. Joseph Modest Mkude, amewataka maafisa usafirishaji kujiunga na bima ya afya kwa wote ili kuwasaidia kukabiliana na changamoto za kiafya hususan wakati wa ajali. Mhe. Mkude pia amejitolea kuchangia vikundi 10 vyenye watu sita sita, endapo mfumo wa bima ya afya utaruhusu kusajili watu hao kutoka vikundi tofauti.
âKw upande wa jeshi la polisi inspecta mzirai usalama wa barabarani amesema wamepokea maelekezo yote ya mkuu wa wilaya wataenda kuzifania kazi â