Savvy FM

Atakaye kamatwa na trampa faini milioni moja

October 22, 2025, 11:15 pm

Mkuu wa Wilaya ya Arusha akiongea na mafundi

Mafundi Gereji zaidi ya 200 Krokoni Waeleza Kero Zao kwa Mkuu wa Wilaya Arusha, DC Mkude Aahidi Utekelezaji na Onyo kwa Wanaotumia Trampa

Na Jenipha Lazaro

Umoja wa Mafundi gereji Krokoni mtaa wa Kitangare, kata ya Kimandolu mkoani Arusha wamemuomba mkuu wa wilaya kuweza kuwatatulia kero zinazowakabili ikiwemo ajira, barabara, kutoa vibali kwa mafundi gereji pamoja na madereva bodaboda wanaoweka trampa.

Sauti ya Ibrahim,Mkurugenzi wa gereji

Kwa upande wa Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Joseph Mkude ambaye ametembelea eneo hilo kusikiliza kero ya mafundi hao, ameweza kutolea ufafanuzi juu ya changamoto zilizoelezwa na kusema tatizo la kutokupewa mikopo, amesema atamuelekeza mtaalamu aje kuwaunganisha umoja wao na kuangalia mikataba ili waweze kupata mikopo ya halmashauri au taasisi zinazotoa mikopo.

Sauti Joseph Mkude,Mkuu wa Wilaya ya Arusha