Savvy FM

Mitaa miwili, viongozi wajadili tuhuma za kimaadili dhidi ya ‘Chinaa’

September 29, 2025, 5:40 pm

Wananchi wa mitaa miwili – Roman Katoliki (rc) na Mbeshere wakiwa kwenye kikao. Picha na Jenipha Lazaro

Wananchi wa Mitaa miwili ya Roman Katoliki (RC) na Mbeshere pamoja na viongozi wa Kata ya Oloirieni jijini Arusha, wamefanya kikao cha dharura kujadili tukio la hivi karibuni la maandamano yaliyofanywa na wananchi kuhusu tuhuma mbalimbali dhidi ya mwanamke mmoja anayefahamika kwa jina Nice Misheri maarufu kama Chinaa.

Na Jenipha Lazaro

Katika kikao hicho kilichohudhuriwa na viongozi wa serikali ya mtaa, viongozi wa dini, pamoja na wananchi wenyewe, malalamiko mbalimbali yaliibuliwa, ikiwemo madai ya unyanyasaji, uporaji wa fedha, na kubambikiziwa bili kubwa zisizoeleweka kwa baadhi ya wakazi wa eneo hilo.

Sauti ya Wananchi wa Mitaa miwili – Roman Katoliki (RC) na Mbeshere wakitoa malalamiko

Kwa upande wake, Nice Misheri maarufu kama Chinaa, amekanusha tuhuma hizo na kusema kuwa yeyote mwenye ushahidi wa tuhuma hizo pamoja na ripoti ya polisi (RB), ajitokeze hadharani.

Sauti ya Nice Misheri/Chinaa mbele wa wananchi

Viongozi wa mitaa hiyo kwa kushirikiana na mtendaji wa Kata ya Oloirieni, wamewataka wananchi kuwa na subira na kutoa ushirikiano wakati huu ambapo wanajiandaa kukaa kwenye kikao maalum cha ulinzi na usalama wa Kata, ili kujadili kwa kina sakata hilo na kutoka na maamuzi yenye maslahi ya pande zote.

Sauti ya viongozi wa Kata na Mitaa husika wakiwa kwenye kikao

Katika hatua nyingine, Jeshi la Polisi kupitia Inspekta Nyamweru Andrea Kasato, amewatahadharisha wananchi dhidi ya kujichukulia sheria mkononi, na kusisitiza kuwa mamlaka za usalama zinaendelea kulifanyia kazi suala hilo kwa mujibu wa sheria na taratibu.

Sauti ya Inspekta Nyamweru Andrea Kasato