Savvy FM

Ndege nyuki kuleta mapinduzi sekta ya kilimo nchini

September 3, 2025, 2:47 pm

Picha ya ndege nyuki(drone).Picha na Shayo

Kampuni ya Mati Super Brands Ltd kupitia kampuni tanzu Mati Technologies imekuja na teknolojia ya kisasa ya Ndege nyuki (drone) kwa ajili ya sekta ya kilimo na huduma nyingine za kijamii ili kuongeza ufanisi.

Na Mussa Kinkaya

Mkurugenzi Mtendaji wa Mati Group of Companies David Mulokozi, amesema kampuni hiyo imeamua kuwekeza kwenye teknolojia ya drone zitakazotumika kunyunyizia dawa mashambani, kupima maeneo, kupanda mbegu, kusafirisha mizigo, kusaidia kaguzi mbalimbali

Sauti ya David Mulokozi,Mkurugenzi Mtendaji wa Mati Group of Companies

Katibu tawala mkoa wa Manyara Mariam Muhaji, amesema mkoa wa Manyara utakuwa wa kwanza kwa Afrika kuwa na kiwanda cha drone hali itakayopandisha hadhi ya mkoa.

Sauti ya Mariam Muhaji,Katibu tawala mkoa wa Manyara

Afisa Ushirika kutoka ofisi ya msajili mkoa wa Manyara, Godamen Merinyo, amesema teknolojia hiyo ni mkombozi mkubwa kwa wakulima, hususan katika mazao kama mbaazi ambayo mara nyingi hukua kwa urefu na kufanya upuliziaji wa dawa kuwa ngumu na wa gharama kubwa. 

Sauti ya Godamen Merinyo,Afisa Ushirika kutoka ofisi ya msajili mkoa wa Manyara