Savvy FM

Wakulima Kivul walia na miundombinu

July 18, 2025, 2:47 pm

Mwananchi wa kijiji cha Kivul akiondoa mabomba yalikuwa yamezuia mifereji ya maji

Wakulima wa Kijiji cha Kivul, kitongoji cha Olmatejo jijini Arusha, wameiomba serikali kuwasaidia kuboresha miundombinu ya kilimo hasa ya maji ya umwagiliaji ambayo imekuwa changamoto kubwa kutokana na mvua.

Na Jenipha Lazaro

‎Wakizungumza wakati wa zoezi la kurekebisha mifereji na mabomba ya maji kwa ajili ya kilimo, wamesema kuwa mmonyoko wa udongo kwenye mto unaotenganisha vitongoji hivyo umeharibu miundombinu iliyokuwepo na kuzuia maji kufika upande wa pili wa mashamba yao.

Sauti za wananchi wa kijiji cha Kivul Olmatejo

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Peter Elias, amesema licha ya baadhi ya mamlaka kufahamu hali hiyo, bado hawajapata msaada wowote, jambo linalohatarisha usalama wa watoto wanaotumia maeneo hayo kuvuka mto.‎

Sauti ya Mwenyekiti wa Kijiji Peter Elias