Savvy FM

Wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za uongozi

July 12, 2025, 10:57 am

Kiongozi wa ACT Wazalendo Doroth Semu akizungumza katika studio za Savvy FM. Picha na Mariam Mallya

Wanawake nchini wametakiwa kuacha hofu na kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ikiwemo Urais, ubunge na udiwani.

Na Mariam Mallya

Kiongozi wa Act Wazalendo ambaye pia ametia nia ya kugombea nafasi ya Urais kwa tiketi ya chama hicho Doroth Semu ameyasema hayo wakati akiwa katika studio za Savvy FM ambapo amesema wanawake wanaweza hivyo wajitokeze kuchukua fomu.

Sauti ya Kiongozi wa Act Wazalendo Doroth Semu

Doroth amesema moja ya sera ya Act Wazalendo ni 50-50 hivyo wanamtazama mwanamke kama mtu ambaye anaweza kufanya mambo makubwa ya kimaendeleo katika nchi .

Sauti ya Kiongozi wa Act Wazalendo Doroth Semu

Kiongozi huyo wa Act Wazalendo amesema chama hicho kimejidhati kuweka wagombea bora kwenye nafasi zote na kuhakikisha wanaweka ilani bora itakayojibu changamoto za wananchi.

Sauti ya Kiongozi wa Act Wazalendo Doroth Semu