Radio Kwizera

Wasimamizi waonywa dhidi ya upendeleo wa kisiasa

August 4, 2025, 6:54 pm

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Muleba Kusini na Muleba Kaskazini Bw. Yona Chalugamba akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa wasimaizi wasaidizi wa uchaguzi 86 ngazi ya kata. Picha na Shafiru Athuman

Wasimamizi wanatakiwa kufuata sheria, taratibu na miongozo ya Tume Huru ya Uchaguzi kwa kushirikisha vyama vyote vya siasa vyenye usajili kamili katika hatua zote kuepuka migogoro

Na Shafiru Athuman- Muleba, Kagera

Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya Kata Wilayani Muleba Mkoani Kagera wametakiwa kufanya utambuzi wa vituo vya kupigia kura kubaini mahitaji maalum ya vituo husika ili uchaguzi ufanyike kwa uhuru na amani.

Baadhi ya Wasimamizi wa Uchaguzi ngazi ya Kata wilayani Muleba wakiwa katika mafunzo kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025. Picha na Shafiru Athuman

Hayo yameelezwa leo hii na Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Muleba Kusini na Muleba Kaskazini Bw. Yona Chalugamba wakati ufunguzi wa mafunzo kwa wasimaizi wasaidizi wa uchaguzi 86 ngazi ya kata.

Bw. Chalugamba amesema kuwa wasimamizi wanatakiwa kufuata sheria, taratibu na miongozo ya tume huru ya uchaguzi kwa kushirikisha vyama vyote  vya siasa vyenye usajili kamili katika hatua zote kuepuka migogoro ili uchaguzi ufanyike uhuru na amani.

Sauti ya Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Muleba Kusini na Muleba Kaskazini Bw. Yona Chalugamba akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa wasimaizi wasaidizi wa uchaguzi 86 ngazi ya kata

Aidha mafunzo hayo yameambatana na kiapo cha kutunza siri za usimamizi wa uchaguzi   kiapo cha kujitoa uanachama wa chama chochote cha siasa kilichotolewa na Hakimu Mkazi Mkuu na Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Muleba Daniel Nyamkerya.

Baadhi ya Wasimamizi wa Uchaguzi ngazi ya Kata wilayani Muleba wakiwa katika mafunzo kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025. Picha na Shafiru Athuman