Radio Kwizera

Serikali yatoa zaidi ya bil 100 kukuza ajira nchini

July 8, 2025, 8:19 pm

Kaimu Mkurugenzi idara ya ajira na ukuzaji ujuzi kutoka ofisi ya waziri mkuu kazi, vijana, ajira na watu wenye ulemavu Bi. Elana Nchimbi akizungumza na vikundi vya wachimbaji wa madini mkoani Geita. Picha na Samwel Masunzu.

Kaimu Mkurugenzi idara ya ajira na ukuzaji ujuzi kutoka ofisi ya waziri mkuu kazi, vijana, ajira na watu wenye ulemavu Bi. Elana Nchimbi amesema hayo akiwa mkoani Geita katika hitimisho la mafunzo kwa wachimbaji wa madini mkoa wa Geita.

Na Samwel Masunzu Geita.

Serikali imetoa kiasi cha zaidi ya shiligi bilioni 100 kwaajili ya kutoa mafunzo kwa makundi mbalimbali ili kukuza sekta ya ajira nchini.

Kaimu Mkurugenzi idara ya ajira na ukuzaji ujuzi kutoka ofisi ya waziri mkuu kazi, vijana, ajira na watu wenye ulemavu Bi. Elana Nchimbi amesema hayo akiwa mkoani Geita katika hitimisho la mafunzo kwa wachimbaji wa madini mkoa wa Geita.

Samweli Masunzu kutoka Geita anao undani wa taarifa hii.

Sauti ya Samwel Masunzu mwandishi wa Radio Kwizera kutoka Geita akiripoti YALIYOJIRI
Baadhi ya vikundi wakiwa katika hitimisho la mafunzo kwa wachimbaji wa madini mkoa wa Geita. Picha na Samwel Masunzu.