Vwawa FM Radio

Utata wa zawadi za bibi au bwana harusi wajadiliwa

June 5, 2025, 4:36 pm

picha ya mtandaoni

Ni kuhusu umiliki wa zawadi ya ardhi au  gari

Na Pili Mwang’osi

Vijana wanaotarajia kuoa ama kuolewa  wametakiwa kutambua kuwa zawadi wanazopewa kwenye sherehe ni hazina ya wanandoa wote.

Mchungaji wa Kanisa la Moravian,Ushirika wa Isangu, Tabson Mgala maarufu Walola Bwana, amesema hayo alipozungumza na Vwawa Fm iliyotaka kujua maoni yake kuhusu zawadi hizo.

Vwawa Fm imeomba maoni ya mchungaji huyo baada  ya kuwepo kwa mkanganyiko wa nani anamiliki kati ya mume na mke.

Amesema zawadi za mali yakiwemo mashamba, nyumba na Magari yanayotolewa zawadi wakati wa sherehe za kumuaga binti ( send off)  au harusi yenyewe.

Mchungaji Walola Bwana amesema kijana wakiume na wa kike wakifunga ndoa mali zote zitamilikiwa na wote, haijalishi uwezo wao binafsi na kwamba kama mmoja wao atafariki, wazazi hawana mamlaka ya kuingilia mali Hizo.

sauti ya Mchungaji Tabson Mgala

Aidha amesema wazazi wanapotoa zawadi  kwa binti yao hawapaswi kuzidai  kwani mali hizo zinabaki kwa wanandoa husika.

sauti ya Mchungaji Tabson Mgala

Lakini  Mwanasheria,  Lusungu Ndawala wa Mbozi  amesema binti anapopewa zawadi za mali au kimiliki kama vile uwanja, nyumba au gari anayo mamlaka ya kuandika umiliki wa mali hizo.

sauti ya Mwanasheria,  Lusungu Ndawala

Baadhi ya wazazi  mjini Vwawa akiwemo Anangisye Kamendu, wametoa maoni yao kuhusu suala hilo.

sauti ya Baadhi ya wazazi