Vwawa FM Radio

Bodaboda chanzo cha migogoro katika jamii

April 24, 2025, 9:06 am

Mmoja wa waendesha bodaboda katika mji wa Vwawa.

Waendesha bodaboda wanatajwa kuvujisha siri za wateja wao

Na Mkaisa Mrisho

MBOZI

Baadhi ya watumiaji wa vyombo vya usafiri maarufu kama Bodaboda wilaya ya Mbozi Mkoani Songwe wamelalamikia baadhi ya waendesha vyombo hiyo kuvujisha siri za wateja wao kwa watu wengine.
Wakizungumza na Vwawa Fm Radio April 15, 2025 wamesema tabia hiyo inaweza kuleta migogoro katika jamii hivyo kuwasihi kuheshimu kazi yao kama kazi nyingine za kuwaingizia kipato.

Sauti za wananchi

Kwa upande wao dereva bodaboda wamesema kuna baadhi ya madereva wanavujisha siri kutokana na abiria wao kukiuka makubaliano.

Sauti ya waendesha pikipiki

Mtaalamu wa masuala ya sheria Saduni Aizak amesema kuvujisha siri za mtu mwingine ni kosa la kisheria, akifafanua amesema.

Sauti ya Saduni Aizak akifafanua zaidi