Uyui FM

Tai sio kigezo cha kuhudumiwa-RC Chacha

2 July 2025, 12:11 pm

Mkuu wa wilaya ya Tabora akiapa kwaajili ya kuanza majukumu. Picha na Mohamed Habibu

”Huitaji kujua mtu ametoka wapi au ni nani,akikukuta ofisini mhudumie” RC Chacha

Na Zabron George

Mkuu wa mkoa wa Tabora Paul Chacha, amewataka wakuu wa wilaya walioapishwa kufanya kazi kwa weledi na kutatua changamoto za wananchi bila ubaguzi.

Mkuu wa mkoa Chacha amesema hayo baada ya hafla ya uapisho kwa wakuu wa wilaya za Sikonge na Tabora katika ukumbi wa mtemi Isike Mwanakiyungi Manispaa ya Tabora.

Sauti ya RC Chacha
Mkuu wa mkoa akizungumza na viongozi pamoja na Wakuu wa Wilaya.Picha na Mohamed Habibu

Mkuu wa wilaya ya Tabora  Upendo Wella na mkuu wa Wilaya ya Sikonge Thomas  Myinga wameahidi kwenda kutatua kero za wananchi.

Sauti za Wakuu wa Wilaya walioapishwa
Mkuu wa wilaya ya Sikonge akiapa kwaajili ya kuanza majukumu.Picha na Mohamed Habibu

Katibu Tawala mkoa wa Tabora Daktari John Mboya amesema ili kazi ifanyike vizuri ni muhimu viongozi kufuata sheria na taratibu zilizowekwa.