Unyanja FM

Mamba kitoweo kwa jamii ya Nyasa

May 26, 2025, 12:49 pm

Wakati maeneo mengine wanamuona mamba kama mnyama mkali lakini sivyo kwa wilaya ya nyasa ambako baadhi ya sehemu amefanywa kitoweo na wahusika kufurahia ladha yake

Na Mussa ndonde

Hayo yameelezwa  na wananchi wa kijiji cha nangombo kitongoji cha tembwe kinachopitiwa na mto luhekei unaomwaga maji yake maji yake kwenye ziwa nyasa.

 Wamesema baadhi ya watu wilayani humo hutumia kama kitoweo huku wengine wakibainisha ladha ya nyama ya mnyama huyo.

sauti ya wananchi wilayani nyasa

JOSEPH MAHAYI ni mkazi wa kitongoji cha luhekei kwa upande wake amekiri watu wanatumia mamba kama kitoweo ila kuna taratibu ambazo zinafuatwa ili kukamilisha zoezi hilo.

MAHAYI amesema  baada ya  kumtega na  kumkamata  huitwa kiongozi wa kijiji  kuthibitisha ukamatwaji wa mamba  huyo na kumtoa nyongo ambayo husambalatishwa kwenye  maji.

Tukio hilo hushuhudiwa na wananchi maana nyongo ni sumu na haipaswi kumilikiwa na mwanajamii

sauti ya Mahayi mkazi wa kijiji cha nangombo wilayani nyasa

Pamoja na mamba kufanywa kitoweo  wilayani nyasa wakazi waishio maeneo hayo hawajawai fanya nyama ya mamba kuwa biashara